Lord Eyes:- Atoa ushauri kwa Chid Benz asipagawe kwani yeye bado ni msanii mkali sana... - Jumaa Lunduno

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, 7 November 2016

Lord Eyes:- Atoa ushauri kwa Chid Benz asipagawe kwani yeye bado ni msanii mkali sana...

Image result for lord eyes fiesta arusha

Rapa Mkali anaeiwakilisha A-Town_Arusha Lord Eyes kutoka katika kundi la Weusi amefunguka na kumtaka msanii Chid Benz_Chuma kutopagawa kwani yeye bado ni msanii mkali sana mwenye uwezo wa hali ya juu.

Hivyo anazidi kumuombe kwa Mungu ili aweze kutoka katika mambo ambayo yanamchanganya pia amemkumbusha kuwa anapaswa kumuomba Mungu kwani kila jambo linawezekana.

Lord Eyes alisema hayo kupitia kipindi cha eNEWZ na kusema kuwa Chid Benz_Chuma asisikilize sana maneno ya watu bali azidi kumuomba Mungu amsaidie kwani kila jambo linawezekana katika dunia hii.

''Na Pia namuombea kwa Mungu Chid Benz a.k.a Chuma_ King Kong namwambia nini asipagawe yaani yeye ni MC mkali sana hivyo asipagawe, namwambia asipagawe najua hajapagawa ila asipagawe, siyajui maisha yake kwa sasa lakini ni mwanangu namuombea Mungu kwani sijamuona siku nyingi nina uhakika atakuwa ‘fresh soon as possible’ kwa Mungu kila kitu kinawezekana namkumbusha pia amuombe sana Mungu'' alisema Lord Eyes
 Image result for chidi benz chuma
Chid Benz a.k.a Chuma

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here