Msaga Sumu: ‘Iga Tena’ siyo dongo kwa mtu yeyote - Jumaa Lunduno

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday 24 October 2016

Msaga Sumu: ‘Iga Tena’ siyo dongo kwa mtu yeyote

 
Mkali wa muziki wa uswazi, anayejiita ''Mfalme wa Uswahili'' Msaga Sumu amesema ngoma yake mpya aliyoipa jina la Iga Tena siyo dongo kwa mtu yeyote, bali ni ujumbe wa kawaida unaotokana na maisha kila siku ya watanzania.

Msaga Sumu ambaye amejitambulisha katika game kupitia muziki wa singeli ametoa ufafanuzi huo wakati akiitambulisha rasmi video ya wimbo huo, kupitia kipindi cha FNL, cha EATV, na kuongeza kuwa huo ni ujumbe kwa watu wote ambao wamekuwa na kawaida ya “kukopi” vitu vya watu bila kuumiza vichwa wala kutambua kazi ya muanzilishi.

Akizungumzia video hiyo, Msaga Sumu amesema ameamua kuwa serious katika muziki na ndiyo maana amefanya kitu kikubwa zaidi katika video hiyo ambayo ameonesha mazingira halisi ya uswahilini.

Kuhusu yeye kufunikwa na baadhi ya wasanii wa singeli walioshika chati hivi sasa, Msaga Sumu ameendelea kusisitiza kuwa yeye ndiye baba wa muziki wa singeli na hakuna mtu atakayeweza kumfunika.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here