P THE MC {Mawenge} Amefunguka Maneno haya baada ya Ngoma ya K ni K Kutoka - Jumaa Lunduno

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday 22 December 2016

P THE MC {Mawenge} Amefunguka Maneno haya baada ya Ngoma ya K ni K Kutoka

 
Mkali Hip hop toka TamaduniMuziki, P the Mc amepiga story na 255 kuhusu mabadiliko yanayoendelea kwa sasa kwenye game ya muziki wa bongo ambayo yeye anasema ni kama kufelisha game yaani sio mabadiliko mazuri.

P the Mc ameongea haya kufuatia release ya ngoma ya Bagdad na Roma ft Snura “K ni K”, P the Mc anasema
''mabadiliko waliyo yafanya kimuziki ni mazuri kwa fikra za kujipatia mashabiki tofauti lakini sina uhakika kama wale mashabiki wao wa mwanzo watapenda au la, unaweza ukaongeza mashabiki 8 alafu ukapunguza 10, nikiwa kama msanii nasema sio mabadiliko chanya”

P the Mc ambaye anatarajia kuachia refix ya All the way up ijumaa hii anasema Bagdad na Roma waliwahi kufanya ngoma ya pamoja “Una Akili Wewe” ikafanya vizuri na mashabiki wakaipokea vizuri
waliweza kufanya wimbo wa una akili wewe katika maadhi yao ya kila siku na ikawa poa tu, sio lazima kuhama misingi”


Ngoma mpya ya P the Mc All the way up Refix itakua exclusive hapa hapa siku ya ijumaa so stay tune.
P Themc 20161222_093813

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here